Kikosi cha Taifa Stars bado kinajengwa na kinaendelea kukuwa siku hadi siku hivyo kinahitaji muda wa kutosha kwa waxchezaji kuwa pamoja na kufanya kazi pamoja ingawa matarajio yake ilikuwa ni kushinda mechi dhidi ya Uganda .
"Ninaiamini timu yangu, bado ni timu nzuri... kufungwa kwetu ni moja ya makosa ya kimchezo na hivyo siwezi kuwalaumu sana wachezaji. Hakikuwa kikosi kibaya," alisema Kim ambaye awali alikuja nchini na kupewa kibarua cha kufundisha timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (U-20) kabla ya kupandishwa baadaye kufuatia kuondoshwa kwa mtangulizi wake, raia mwenzake wa Denmark, Jan Poulsen.
0 comments:
Post a Comment