Thursday, June 20, 2013

NIKIWA COASTAL NITAFANYA MAKUBWA-UHURU SELEMAN


Mchezaji Uhuru Seleman aliekuwa akiichezea timu ya Azam Fc kwa msimu uliuopita wa Ligi kuu Bara kwa sasa Amejiunga na Timu ya Coastal Union ya jijini Tanga kwa mkopo akitokea Azam FC alipokuwa akisakata Kabumbu kwa msimu uliokwisha wa Ligi.


Uhuru kabla ya kutangaza rasmi kujiunga na Kikosi Hicho cha Coastal Union kwa ajiri ya Msimu ujao wa ligi alifanya utafiti ili kujuwa anapaswa kwenda kucheza timu gani na kwanini anakwenda katika timu hiyo na alifanya hivyo wazi kulinda na kukuza kipaji chake kama mchezaji,moja ya timu ambazo alionesha kuhitaji kwenda ilikuwa ni Simba Sports Club,Coastal Union pamoja na Azam.

Nakumbuka Uhuru aliandika “Leo Mei 24 nimetimiza miezi sita tangu nilipotua Azam, naomba mnisaidie nienda wapi Coastal Union, Simba au Azam.” Baada ya wadau kumpa ushauri wengi wao walimshauli kurudi Simba Sports Club na haijawa hivyo niklitaka kujuwa sababu za yeye kutojiunga na Timu yake ya Simba aliyokwisha ichezea msimu wa Nyuma

Na majibu yake yalikuwa hivi “ni kweli9 nilitaka ushauri kutoka kwa mashabiki wangu ambao wao ndio wanaonipa moyo na hamasa ya kufanya kazi nzuri zaidi na walinishauri na nilichukua maamuzi yao ila nimeamua kujiunga na Coastal Union ya mjijini Tanga kwa kuwa natambua nikiwa Coastal Union nitafanya makubwa kisoka kwa kuwa naamini nitakuwa na nafasi ya kuonesha uwezo wangu”




0 comments:

Post a Comment