Friday, June 21, 2013

MAD ICE KUZINDUA WASIWASI JUMAPILI AKIWA NA FID Q

Msanii Mad Ice anataraji kuzindua single yake mpya inayokwenda kwa jina la wasiwasi siku ya Jumapili ya Tarehe 23 katika Ukumbi wa Club Bilicanas  katika usiku wa Bongo Stars usiku

Usiku huo utasindikizwa na mtu mzima Fid Q anaewaikilisha jiji la Mwanza kiburudani kinyumbani na kuwakilisha Taifa katika Muziki Kiujumla.

Mad Ice ataachia single yake hiyo baada ya kukaa kmya kwa muda mrefu katika Game la muziki kwa hapa nyumbani japo alikuwa kaiendelea kufanya muziki  akiwa nje ya Nchi


“Nina mashabiki kila idara, hilo sijalisahau na kamwe siwezi kuwasahau kama wengi wasemavyo. Sasa mchongo uko hivi... Jumapili hii ya tarehe 23, tukune pale CLUB BILICANAS katika uzinduzi wa single yangu mpya "Wasiwasi". Nitasindikizwa na mzee mzima FID Q, usikose show kali na ya ukweli”

0 comments:

Post a Comment