Friday, May 10, 2013

SODA HAINA SUMU-TFDA





Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imetoa taarifa kuwa kinywaji cha Soda hakina sumu kama ambavyo taarifa zilivyozagaa hivi karibuni katika mitandao ya jamii nchini zikionesha Athari ya kinywaji hicho kwa mtumiaji kuwa kina sumu.

Mamlaka inamashaka na taarifa iliyotolewa kwa sababu haidhani kama ilitolewa kwa kuzingatia misingi ya kisayansi .

Mamlaka inawatoa hofu watumiaji wa kinywaji Hicho kuwa Soda ni bidhaa ya chakula ambayo inatumika duniani kote na inatengenezwa kuzingatia viwango vya ubora na usalama kwa matumizi.

TFDA Soda zote zilizosajiliwa zimepitia katika mchakato ambao unatoa uhakika juu ya usalama wake kwa lengo la kulinda afya ya Binadamu .

0 comments:

Post a Comment