Wednesday, May 22, 2013

FRANCIS CHEKA AMECHOMOA SHUTUMA ZA KUTUMIA UCHAWI



Bondia wa Francis Cheka amesema kuwa mchezo wa ngumi unahitaji maandalizi zaidi na si uchawi kama ambavyo baadhi ya watu wanavyomtuhumu kuwa inawezekana anatumia uchawi katika michezo yake hiyo ya ngumi.

Cheka amesema kuwa kama Ubondia ungekuwa unaambatana na uchawi basi kuna mabondia kutoka Sumbawanga,Tanga basi wangekuwa wanafika mbali zaidi katika mchezo huo lakini kwa kuwa ngumi si uchawi ndio maana hawajaweza hata kupata ubingwa ambao yeye amepata katika mchezo huo.

watu wanasema kuwa kuna watu wanatumia uchawi katika kushinda,hakuna jambo kama hilo katika mchezo wa ngumu,ngumi huitaji mazoezi ya kutosha na kujianda vya kutosha dhidi ya mpinzani wako,ingekuwa ngumi ni uchawi basi mabondia kutoka Tanga,Sumbawanga,Kigoma wangekuwa wanashinda kila siku.

Bondia francis cheka alithibitisha kuwa hana mpinzani Tanzania baada ya kumtwanga bondia mashali katika round ya 10 na kumpelekea kupoteza fahamu kwa muda na kushindwa kuendelea na pambano hilo.

0 comments:

Post a Comment