Msanii Kutoka Senegal alieweka makazi yake Nchini Marekani
kwa sasa Akon leo amempongeza Raisi Mteule wa kenya Uhuru Kenyatta baada ya kufika
katika uwanja wa mpira ulijaa maelfu ya wafuasi wa Kenyatta.
Akon amesema kuwa Hongera Uhuru Kenyatta kwa nafasi mpya ya
Uraisi,ulimwengu unajivunia Kenya kwa mabadiliko ya amani.hili ni kubwa
sanaa.Nipo hapa Hong Kong na hakuna jingine zaidi ya Habari ya Kenya.
Natamani ningekuwepo hapo na kushudia sherehe hizo za
kuapishwa.
“Congratulations Uhuru Kenyatta on your new presidency. The
world is proud of Kenya and its peaceful transition. This is big. I'm in Hong
Kong and it's all over the news. I wish I could be there to Witness. AKON”.
Kenyatta mwenye umri wa miaka 51 ni mtoto wa rais wa
kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta. Ushindi wake wa asilimia 50.07 katika uchaguzi
wa tarehe 4 Machi ulihalalishwa na Mahakama ya Juu baada ya pingamizi
lililowekwa na Waziri Mkuu anayemaliza muda wake, Raila Odinga, kutupiliwa
mbali na mahakama hiyo.
Kenyatta anayekuwa rais wa nne wa taifa hilo
la Afrika ya Mashariki tangu lilipopata uhuru wake kutoka Uingereza mwaka 1963,
anakuwa rais wa pili barani Afrika kuwa madarakani hali anakabiliwa na
mashitaka kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kwa tuhuma za kusaidia
kuchochea ghasia za kikabila zilizoukumba uchaguzi wa urais wa Kenya wa mwaka
2007.
Msanii Kutoka Senegal alieweka makazi yake Nchini Marekani
kwa sasa Akon leo amempongeza Raisi Mteule wa kenya Uhuru Kenyatta baada ya kufika
katika uwanja wa mpira ulijaa maelfu ya wafuasi wa Kenyatta.






0 comments:
Post a Comment