Tuesday, May 21, 2013

PROFESA JAY AFUATA NYAYO ZA SUGU AJIUNGA NA CHADEMA


Msanii wa muziki wa bongo fleva Joseph Haule alimarufu kama Profesa J ameamua kufuata nyayo za mwanamuziki mwenzake Joseph Mbilinyi kwa kuingia rasmi katika siasa na kuchukua kadi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA .

Kwa mujibu wa watu wa karibu wa Jay wamesema kuwa hayo ni maandalizi ya uchaguzi wa mwaka 2015 ingawa Jay mwenyewe amesema kuwa amechukua kadi ya Chadema kama mwanaharakati wa siasa na kutaka kuendeleza harakati zake hizo kupitia chama hicho.

Masaa kadhaa kabla ya Profesa Jay kuchukua kadi ya Chadema alidai kuwa muda mrefu watu walikuwa wakitaka kujua yeye ni chama gani kutokana na kumuona akihusika kisaniii katika baadhi ya vyama hivyo walitaka kujua yeye ni chama gani.

Hivyo aliamua kuandika katika mtandao wa kijamii kuwa“Mmeniuliza sana kwamba mimi ni CHAMA gani jibu litapatikana Muda sio mrefu!! Still in Dodoma STAY TUNED!!!”

Baada ya ku stay Tuned ndipo alipoonyesha mapenzi yake kwa chama cha Demokrasia na Maendeleo kama ionekanavyo katika picha.





0 comments:

Post a Comment