Yakiwa
yamebakia masaa kadhaa kwa watani wa Jadi Simba na Yanga kukutana
katika Uwanja wa Taifa na kuoneshana makli yao uwanjani homa ya soka
imeeanza kutawala kwa mashabiki hata viongozi wa Club hizo mbili
kutokana na ukweli kwamba kila Club imekamia kushinda mechi ya kesho
ili kuonesha ukali na kuthibitisha umahiri wake nakuoneshana mabavu
ya kijadi jadi yale.
Kwa
namna moja au nyingine mechi kati ya watani hawa si nyepesi hata
kidogo kwani kila Club imekamia kufanya vizuri hivyo utakuwa ni
mchezo wa kukamiana katika kutafututa ushindi kwa hili kila mmoja
anajiuliza nani atamwanga pombe ya mwenzake ni Simba au Yanga.
Mchezo
kati ya watani wa jadi hawa utachezeshwa na mwamuzi Martin Saanya
kutoka Morogoro akisaidiwa na washika vibendera Samuel Mpenzu kutoka
Arusha, Jesse Erasmo kutoka Morogoro huku mwamuzi wa akiba akiwa
Hashim Abdallah kutoka Dar es salaam.
Kocha
Mkuu wa Yanga Ernie Brandts amesema kikosi chake kipo fiti, kiakili,
kifikra, kiafya na morali ya wachezaji ni ya hali ya juu hivyo wana
kila sababu ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo kwakua Yanga kwa
sasa ina kikosi bora kuliko timu zote katika ukanda wa Afrika
Mashariki.
Tabiri ushindi wa kesho kati ya watani wa jadi hawa.







0 comments:
Post a Comment