Thursday, December 5, 2013

WAZIRI MKUU AMEMUUMBUA ZITTO KABWE BUNGENI

Waziri mkuu Mizengo amemuumbua Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh Zitto Kabwe na kudai kuwa ameudanganya Umma kwa kutoa taarifa sisizo sahihi juu
ya Mshahara wake kama waziri mkuu,Mizengo Pinda ameweka wazi mshahara wake na kusema kuwa analipwa mshahara wa milioni 6, mshahara ambao ni pamoja na posho ya mke wake.

Mwezi uliopita Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh Zitto Kabwe akiwa anahutubia wananchi wa Mji wa Mpanda katika viwanja vya maridadi alifunguka na kusema kuwa waziri mkuu anapata mshara wa shilingi milioni 26 kwa mwezi na kila kitu anapata bure.

Lakini Mizengo Pinda amekanusha na kusema kuwa haelewi hiyo taarifa Zitto aliyoitoa kwa Wananchi imetoka wapi pia aliongeza kuwa mshahara wake hauna tofauti kubwa sana na mshahara wa Rais, kwani kuwa hautofautiani sana.

Kutokana na hali hiyo Mizengo Pinda amedia kuwa yeye amekuwa ni mkopaji mzuri sana katika Mabenki mbalimbali ili aweze kukidhi haja ya mahitaji yake.

0 comments:

Post a Comment