Tuesday, December 3, 2013

NIYONZIMA ALILIWA YANGA

Kiungo wa Yanga Mnyarwanda Haruna Niyonzima ambaye kwa sasa yupo Nchini Kenya na Kikosi cha Timu yake ya Taifa ya Rwanda AMAVUBI inayoshiriki
mashindano ya kombe la Chalenji ameliliwa na kuonesha kuhitajika Mno katika Kikosi cha Yanga ili kukamilisha baadhi ya Program ambazo Timu hiyo imezianza kujiandaa na Mashindano ya Afrika Mwakani.
 
Kufuatia Mazngira hayo Kocha wa Yanga amemtaka kiungo huyo kurejea kurejea haraka Tanzania ili kujiunga ndani ya kikosi chao kinachojiandaa kwa mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya watani wao wa jadi, Simba.
 

"Kwa kuwa Rwanda tayari imeshatolewa Chalenji, sioni haja Niyonzima kukawia kujiunga na timu yangu (Yanga). Tunakabiliwa na mashindano magumu ya Afrika mwakani, tunatakiwa kujiandaa vizuri na kwa wakati," alisema Brandts.

0 comments:

Post a Comment