Tuesday, December 3, 2013

KOCHA WA YANGA ASAINI MKATABA NDANI YA GARI

Kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts, ameongeza mkataba wa kuendelea Kukinoa Yanga kwa Mwaka Mmoja,Kocha huyo
ambaye jana alisaini Mkataba huo akiwa kwenye Gari yake wakati Timu hiyo ikiendelea na Mazoezi katika Uwanja wa Bora Kijitonyama jijini Dar es Salaam .


Baada ya mazoezi ya timu hiyo kumalizika kwenye uwanja huo majira ya saa tano asubuhi huku kukinyesha mvua, Brandts aliingia kwenye gari lake akifuatwa na Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh ambaye naye aliingia kwenye gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser na kukabidhi mkataba kwa kocha huyo.

Baada ya mchakato kukamilika Kocha huyo alikubali kusaini Mkataba wa kuendelea kukinoa Kikosi cha Yanga..

"Ndiyo, nimesaini mkataba mpya na Yanga mbele ya Meneja wa Timu (Saleh). Kama kawaida yangu, sihitaji mkataba mrefu zaidi, hivyo nimeingia nao mkataba wa mwaka mmoja tu,"




0 comments:

Post a Comment