Sunday, December 1, 2013

MBUYE TWITE ATIMULIWA

 Mchezaji Kiraka  Yanga Mnyarwanda Mbuyu Twite amechomolewa katika Kikosi cha Timu ya Taifa ya Rwanda kutokana na kukaidi Agizo lililomtaka kurudi
Rwanda katika Timu ya Taifa kuisaidia timu yake ya Taifa dhidi ya Mali. 

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Rwanda Eric Nshimiyimana, amesema hana mpango na mchezaji huyo baada ya kumwita kwenye mechi dhidi ya Mali akakaidi na kuzima simu.

Ni tabia mbaya kwa mchezaji kuitwa na kukaidi, kocha hawezi kumnyenyekea mchezaji mmoja kwenye timu ya Taifa. Nafasi ya Mbuyu imeshazibwa na vijana wadogo ambao wanafanya kazi kikamilifu.

Hatuwezi kuendelea kuendekeza hizo tabia, tuna wachezaji kama wanne wadogo ambao wanaweza kufanya kazi vizuri kabisa, hakuna haja ya kuangaika na Mbuyu.”

Kutokana na mazingira hayo kwa sasa Beki huyo anayekipiga katika Klabu ya Yanga hawezi kupata nafasi kirahisi kurudi katika Kikosi cha Taifa katika Timu ya Rwanda.
Source:Mwanaspoti.



0 comments:

Post a Comment