Thursday, November 28, 2013

AFRICAN LYON YAWAVURUGA WACHEZAJI WA YANGA

Timu ya African Lyon ambayo inacheza Ligio Daraja la Kwanza kupitia Viongozi wake umeendelea kuwavuruga baadhi ya Wachezaji wa Yanga ambao wanataka
kusajiliwa na Timu hiyo kwa njia ya Mkopo kutoka Kwa Mabingwa watetezi Yanga.

Siku mbili zilizopita moja ya kiongozi wa Juu ya African Lyon alikuwa na Mazungumzo na Kocha wa Mabingwa Watetezi Yanga baada ya Mazungumzo hayo Kiongozi huyo alitoa taarifa kuwa alifika Uwanjani hapo ilikuzungumza na Kocha huyo juu ya kuwapata wachezaji watano ambao Timu yake inawahitaji.

"Sisi (African Lyon) tuna uhusiano mzuri na Yanga, nimekuja hapa uwanjani kuzungumza na benchi la ufundi la Yanga kuhusu wachezaji wao watano ambao tunataka kuwasajili kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo. Brandts amesema hana tatizo na suala hilo na yuko tayari kuwaachia kwa sababu hawahitaji sana kwenye kikosi chake kwa sasa,"

Kutokana na Taarifa hizi kuwafikia Wachezaji wa Yanga kuna baadhi ya Wachezaji wameonesha wasiwasi na kuwa na hofu huenda wao ndio wakauzwa kwa mkopo kwenda African Lyon kutokana na kutopata nafasi uwanjani kutokana na uwezo wao kuwa chini kidogo dhidi ya wale wanaopata nafasi kucheza Uwanjani.

0 comments:

Post a Comment