Thursday, October 3, 2013

MCHEZAJI WA YANGA HARUNA NIYONZIMA APATA MAJANGA

Kiungo wa Yanga Mnyaruanda Haruna Niyonzima amepata majanga baada ya nyumba anayoishi kuungua kwa moto
usiku wa kuamkia leo maeneo ya Magomeni Makuti Dar es salaam.

Kutokana na kuungua kwa nyumba hiyo iliyokuwa na wapangaji wawili imesababisha hasara na uhalibifu wa vitu mbalimbali hasa zaidi katika Furniture na vitu vya sebuleni vikiwemo Luninga,Radio na vitu vingine vilivyotumika kupamba sebule ya Mchezaji huyo wa Yanga.

Wakati nyumba hiyo ikiwa inateketea kwa moto Haruna Nyionzima alikuwepo ndani ya nyumba hiyo na kusaidiwa na majirani katika kuzima moto huo.

0 comments:

Post a Comment