Monday, October 28, 2013

ALIYEMUUWA MICHAEL JACKSON AMEACHIWA HURU

Aliyekuwa Daktari Binafsi wa Mfalme wa Pop Duniani Michael Jackson ambaye alituhumiwa kusababisha kifo cha Mwanamuziki huyo na kufungwa kifungo cha miaka Minne gerezani amechiwa huru leo.

 
Conrad Murray alituhumiwa kifungo cha miaka Minne Gerezani baada ya kukutwa na hatia ya kusababisha kifo cha Michael Jackson kwa kumdunga Dawa zilizopeleke Kifo cha Jackson .

Ikiwa Miaka Miwili imeshapita toka kukutwa na Hatia ya kuuwa pasipo kukusudia leo ameachiliwa huru baada ya kutumikia kifungo hicho zaidi ya miaka miwili toka alipohukumiwa November 2011 .

Taarifa za Gereza alililokuwa amefungwa Murrays zimethibitisha Kutolewa kwa Daktari huyo hata afisa wa Gereza pia amethibitisha kuwa ameachiwa muda 12:01 Jumatatu.

Michael Jackson alikufa siku ya Tarehe 25 June 2009 baada ya kuzidishiwa dozi na Daktari Murray.
Murray ambaye kwa sasa ana umri wa Miaka 60 alifungwa miaka Minne lakini kubadilika kwa Sheria za California kumepelekea kupunguza kwa vikwazo kwake





0 comments:

Post a Comment