1:14 AM
By Chris Mauki.
Nimekutana na lawama na
malalamiko mengi sana kati ya wapenzi na hata maranyingine
waliojikuta wameshaingia kwenye ndoa na nimeona nivema nitafute jinsi
ya kuwasaidia wenye tatizo hili au kukuwezesha na wewe kumsaidia na
mwingine.
Wako wapenzi wanawake au wanaume ambao tabia yao
nikutafuta namna ya kuzichimba pesa za mpenzi wake kwa namna yoyote
ile.
Mara nyingi wanaume wamekuwa
wakiwalalamikia wanawake kuwa ndiyo wanaojifanya wanapenda kumbe
wanachokitaka ni pesa au unafuu wa maisha kiuchumi kutoka kwa wapenzi
wao wakiume.
Lakini sikuhizi mambo yamekuwa na
uwiano sawa, wako vijana wa kiume pia ambao kazi yao ni kuwalemea
wapenzi wao kila siku kwa mahitaji yasiyoisha.
Leo watasema wanashida hii, kesho
shida nyingine itaibuka, na keshokutwa atakuja na jipya pia. Hali hii
huyafanya mapenzi yakawa butu sana hatakama anayeelemewa hajaweza
kusema kwa uwazi maumivu anayo yapata.
0 comments:
Post a Comment