Waziri wa Uchukuzi, Dk.
Harrison Mwakyembe ametema cheche juu ya sakata la madawa ya kulevya
kupitishwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa JNIA...!
haiwezekani
dawa za kulevya kupitishwa kirahisi katika uwanja huo wakati kuna
vyombo mbalimbali vya serikali kama Usalama wa Taifa, Polisi, Mamlaka
ya Viwanja vya Ndege (TAA), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Idara
ya Uhamiaji na nyingine na wanalipwa mshahara na serikali.
Nilikaa
kimya ili kuvipa muda vyombo vya usalama vijiridhishe na kunipa
taarifa kutokana na sakata hilo kwani ni aibu kwa uwanja wa ndege
wenye jina la Mwalimu Nyerere na nchi kwa ujumla kuchafuka kimataifa
kutokana na watu wachache wazembe.
“Tatizo
hapa siyo mfumo wa mitambo ni uswahili tu ndiyo unaofanyika hapa, leo
nitaitisha mkutano na waandishi wa habari kueleza Watanzania
wanaofanya hujuma na hatua walizochukuliwa, nataka kuvisafisha
viwanja vya ndege ili dawa za kulevya zisipite tena hapo,”
hatua nitakayo chukua itakuwa ni historia na kama wapo watu waliozoea kupitisha dawa za kulevya katika viwanja hivyo labda watafute njia nyingine ya kusafirisha kama ya punda.
hatua nitakayo chukua itakuwa ni historia na kama wapo watu waliozoea kupitisha dawa za kulevya katika viwanja hivyo labda watafute njia nyingine ya kusafirisha kama ya punda.
0 comments:
Post a Comment