FFU WAKIWA WAMEJIPANGA KUWEKA ULINZI MKALI WAKATI SHEIKH PONDA ANASOMEWE MASHITAKA JANA AKIWA HOSPITALI. |
Lakini
siku ya jana badala ya kuhojiwa kama ilivyoelezwa na wakili wake bali
alifunguliwa mashitaka akiwa kitandani katika wodi na hali ilikuwa
hivi.
Wakati
polisi wakimfungulia mashitaka Sheikh Ponda wodini hakuna mtu yeyote
aliyeruhusiwa kuingia wakiwamo waandishi wa habari na wafanyakazi wa
hospitali hiyo.
Taarifa za Sheikh Ponda kufunguliwa mashtaka zilitolewa na wakili wake, Juma Nassoro, ambaye alisema kesi hiyo itakuwa chini ya Hakimu Hellen Riwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu.
Nassoro alisema Sheikh Ponda alisomewa shitaka hilo la kuhamasisha watu kufanya makosa akiwa kitandani Moi ambako anaendelea na matibabu baada ya kudaiwa kujeruhiwa kwa risasi mkoani Morogoro Jumamosi iliyopita.
Taarifa za Sheikh Ponda kufunguliwa mashtaka zilitolewa na wakili wake, Juma Nassoro, ambaye alisema kesi hiyo itakuwa chini ya Hakimu Hellen Riwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu.
Nassoro alisema Sheikh Ponda alisomewa shitaka hilo la kuhamasisha watu kufanya makosa akiwa kitandani Moi ambako anaendelea na matibabu baada ya kudaiwa kujeruhiwa kwa risasi mkoani Morogoro Jumamosi iliyopita.
0 comments:
Post a Comment