Baada
ya ushindi wa magoli 4-1 dhidi ya mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya
Uganda, SC Villa, katika mechi ya kirafiki ya kujiandaa na msimu mpya
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, kocha wa...!
Simba, Abdallah
Kibadeni amedai kuwa kikosi chake kiko tayari kurejesha heshima
iliyopotea msimu uliopita."Nimeridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wangu, yaani kilikuwa tofauti na cha juu ukilinganisha na mechi iliyopita, na hapo niliwakosa wachezaji wawili wa kigeni, ila tayari picha halisi ya kikosi cha kwanza nimeshaipata," alisema Kibadeni ambaye aliibuka kocha bora wa msimu uliopita baada ya kuiongoza Kagera Sugar kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi.
Alisema pia ushindani wa kusaka namba umeongezeka Simba na kwa sasa hana hofu na yuko tayari kuanza kuusaka ubingwa wa ligi ambao unashikiliwa na wapinzani wao, Yanga.
0 comments:
Post a Comment