Kauli aliyoitoa
Waziri mkuu Mizengo Pinda Bungeni mwanzoni mwa mwezi huu ya kuwataka
Polisi kuwapiga Tu raia ambao wanakiuka taratibu na kutofuata Sheria
zitolewazo na Jeshi hilo la Polisi wawapokazini katika kuzuia vitendo
vya Fujo....!
Uchokozi au kuzuia
vitendo vyovyote vinavyoashiria kuvunjika kwa amani,Kituo cha Sheria
na Haki za Binadamu kinatarajia kumfikisha mahakamani Waziri Mkuu
kikimtaka atengue kauli hiyo aliyoisema mbele ya Bunge la Jamhiri ya
Muungano wa Tanzania.
Mwezi uliopita
Pinda katika mkutano wa Bunge la bajeti mjini Dodoma alitoa kauli ya
kulitaka jeshi la Polisi nchini kuwapiga raia wanaokaidi amri halali
ya jeshi hilo wakati aikijibu maswali ya Papo kwa papo kwa Waziri
Mkuu.
Mkurugenzi wa
Maboresho na Utetezi wa LHRC, Harold Sungusia, alisema taratibu zote
za kisheria za kumfikisha Pinda mahakamani zimekamilika na siku
yoyote wiki hii watafungua kesi.
Kiukweli kauli ya Pinda,
imevunja katiba ibara ya 13 na kwamba lazima sheria ichukue mkondo
wake kwa mkumfikisha mbele ya mahakama.
Alifafanua kuwa ibara
ya 100 inayompa kinga mbunge anapotoa jambo lolote bungeni inamweka
kando Pinda, kwa kuwa yeye hakuzungumza bungeni kama mbunge bali
alikuwa anatoa msimamo wa serikali yake.
Alisema
kauli ya Pinda ilikuwa kali na mbaya na kwamba, walimtaka Pinda
aifute siku chache baada ya kuitoa, lakini mpaka sasa amekaidi na
hivyo wameamua kuchukua hatua ya kumfikisha mahakamani ili haki iweze
kutendeka.
0 comments:
Post a Comment