Friday, June 21, 2013

KUMBE NGOMA YA BEN PAUL JIKUBALI AMECOPY SIKILIZA MWENYEWE ORIGINAL VERSION


Nianze kwa kutoa pongezi kwa Ben Paul na Producer wake Lucci kwa kuweza kufanya kazi nzuri ambayo ni inspiration Song kwa vijana wa Kitanzania,Ben paul katika ngoma hiyo ameonesha uwezo wake wa Hali ya juu sana pamoja nae Lucci katika kuikamilisha ngoma hiyo.

Lakini baada ya Ngoma hiyo kufanikiwa na kupokelewa vizuri na jamii kuna ngoma kama hiyo ya Inspiration pia yenye midundo ya ngoma ya Jikubali ya Ben Paul,yenye Idea ya inayoelekeana nay a Jikubali hata Stlye ya Kuimba ambayo ni ya Msanii The Script akiwa amempa Shavu  will.i.am na ngoma inakwenda kwa jina la Hall Of Fame .

 

Sina tatizo na Ben Paul wala Lucci ila tatizo langu lipo katika kitu kimoja kinaitwa Attribution si vibaya kucopy au kurudia ngoma yoyote ile maana hata kwa wenzetu wanafanya hivyo ila unapaswa kusema kuwa hicho kitu ni cha mtu na wewe umekirudia tuu ili hata kama unapata credit kwa kazi hiyo tunakuwa tunajua chanzo chake kipi lakini ndugu zangu hawa wamefanya kazi kama yao na kupiga kimya kama wao ndio wameifanya kazi hiyo mwanzo mwisho.

 

Kwa hili Ben paul na Lucci hamjatenda haki tunaitaji nyinyi muwe mfano wa kuigwa kwa kuwa mnafahamu mambo ya Haki miliki jinsi yanavyokwenda,mna elimu ambayo inaweza kuwasaidia kujuwa hicho mlichofanya,sasa kama nyinyi mnafanya hivyo kina Nanii wafanye nini sas?

 


Nisionekane kama nimewaundia hoja nanyi mshuhudie wenyewe kazi waliyocopy japo kiuwezo Msanii Ben Paul na Lucci wapo vizuri na hakuna anaebisha katika hilo. BOFYA LINK HIII NA UTAJIONEA MWENYEWE.http://www.youtube.com/watch?v=jukv9Q1eR2g

0 comments:

Post a Comment