Tuesday, April 9, 2013

ZITTO AYASHUKIA MAKAMPUNI YA SIMU TANZANIA


Mbunge wa Kigoma Kasikazini Mh Zitto Kabwe ameyashukia makampuni ya Simu kuwa wanapaswa kulipa kodi ya mapato bila kuangalia aina ya uwekezaji walioufanya nchini.

Zitto ameyasema hayo kufuatia Kauli ya serikali waliuoitoa kuwa makampuni ya simu Nchini yanalipa kodi nyingi,kufuatia kauri hiyo Zitto alihoji kodi gani inayolipwa na makampuni hayo? VAT! Nani kasema VAT inalipwa na kampuni?Hii Ni kodi ya walaji kama ilivyo ushuru wa bidhaa (excise duty).

“ Serikali inasema kampuni za simu hazilipi kodi ya mapato Kwa kuwa zimewekeza sana, Tshs 2.5 trilion! Nani kakagua huo uwekezaji? Eti Kwa miaka 5 kodi ya makampuni iliyolipwa Ni Tshs 64 bilioni, ambayo ni wastani  wa Tshs 12 bilioni Kwa mwaka.”

Aliendelea kukaliliwa akisema kuwa kwa Nchi kama Rwanda yenye idadi ndogo ya Wananchi ambapo ukilinganisha na Tanzania ni sawa na wateja ya Kampuni moja ya simu lakini wao Nchi yao ililipwa kodi ya juu zaidi kuliko Tanzania hivyo aliitaka serikali ya Tanzania kuacha Utani na Blah blah katika vitu vya msingi na vyenye masirahi kwa Taifa letu.

 “Rwanda yenye idadi ya watu sawa na wateja wa Vodacom peke yake mwaka 2010 walikusanya corporate tax $14m, Tanzania ilikusanya $1.4m tu. Serikali iache blah blah, ikusanye kodi. TCRA ipewe Nguvu ya kukagua uwekezaji wa makampuni kama ilivyo TMAA kwenye madini. Inatosha sasa

0 comments:

Post a Comment