Saturday, January 12, 2013

BILA MAMA NINGEACHA MUZIKI




Na Kitalima Gerald 

MTAYARISHAJI wa muziki wa Bongo flavor na mmiliki wa Studio ya BURN Records Sheddy Clever Amefunguka na kusema kuwa Bila mama yake mzazi(Rebeca)Angekua ameshakata tamaa na kuachana na masuala ya kutayarisha muziki.

Sheddy Clever amesema hayo kufuatia support kubwa anayoipata kutoka kwa mama yake Mzazi kimawazo na ushauri pindi anapopata changamoto katika kazi yake ya utayarishaji wa muziki na maisha Kiujumla.

“Mama yangu ndio kilakitu na mafanikio niliyopata kimuziki basi mama anamchango mkubwa sana kwani kunakipindi nilipigiwa simu za vitisho mpaka kufikia hatua ya kutaka kuachana na Muziki lakini Bimkubwa alinishauri kusimamia katika kitu nachokiamini nitafanikiwa tu.

Sheddy Clever alietengeneza HITS kama Zilipendwa(Matonya),Mary me(Mavoko) Nivute Kwako (Dyana) Amekua (Pasha$Tunda Man) Ameweka wazi Alikua na Mpango wa kufanya kazi na Diamond Platinum na Mpaka sasa Anaona hizo ndoto Zipo njiani Kutimia kwani teyari amekwisha tengeneza Beat na Diamond Platinum.

AKizungumzia Ushirikiano kati yake na Watayarishaji Wengine wa Muziki Nchini Tanzania Amesema kuna baadhi yao wanaushirikiano mzuri mno lakini wengine ni Tatizo 

CO UDAKU SPECIAL
SHEDDY CLEVER KWA POZI

“Kiukweli kabisa kuna producers kama MAN WALTER Ana roho nzuri sana yeye kanipa support sana kimawazo hata kunifunza vitu vingine, kiukweli Big up kwake lakini kuna baadhi ya producers hawafanikiwi kutokana na Roho mbaya zao.

0 comments:

Post a Comment