Monday, May 20, 2013

WANAVYUO WASUMBULIWA NA KUNGUNI MABWENINI


Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Nairobi wamelalamikia ongezeko la kunguni katika vyumba vya kulala chuoni. Wanasema kunguni wameongezeka mno hasa katika vyumba vya kulala vilivyojengwa kwa mbao, almaarufu 'Prefabs,’ vinavyotumiwa na wanafunzi wapya na wa mwaka wa pili.

Wanasema kunguni wameongezeka mno hasa katika vyumba vya kulala vilivyojengwa kwa mbao, almaarufu 'Prefabs,’ vinavyotumiwa na wanafunzi wapya na wa mwaka wa pili.

Kulingana na wanafunzi hao, vyumba hivyo vimevamiwa na kunguni kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi na kupelekea hali mbaya ya usafi.

Kunguni wamekuwa wengi sana msimu huu,” alisema Bw Joseph Maina kiongozi wa wanafunzi chuoni.
Wanafunzi walishtumu usimamizi wa chuo hicho kwa kuzembea katika kudumisha usafi wa wanafunzi wanaozidi kuongezeka kila mwaka.

Chumba kimoja hutumiwa na wanafunzi watano au hata zaidi. Kuna msongamano mkubwa wa wanafunzi unaofanya usafi kudorora na maisha katika vyumba hivyo kuwa magumu,” akasema Dominic Thuva mwanafunzi wa mwaka wa pili.

Wanafunzi wapya waliokuwa wakisajiliwa Jumatatu walionekana wakikagua godoro hizo pamoja na wazazi wao kabla ya kuanza kuzitumia.

Baadhi ya wanafunzi pia walihusisha kunguni hao na kutobadilishwa kwa godoro zilizotumiwa kwa muda mrefu.

0 comments:

Post a Comment