Thursday, April 25, 2013

MAMA MONALISA ACHUMBIWA NA KUVALISHWA PETE

Msanii wa maigizo na Tamthilia nchini Natasha ambae pia ni MAMA Mzazi wa Msanii wa Maigizo Monalisa hivi karibuni alivalishwa pete ya Uchumba na kutalajia kufunga Ndoa siku za mbeleni.

Natasha akifunguka hayo leo katika kipindi cha Redio leo amesema kuwa anafurahia hali ya kuwa mchumba wa mtu na kutarajia kufunga ndoa siku za usoniii alipohojiwa kuwa mwanae Monalisa amelipokeaje suala hilo alisema kuwa mwanae amefurahi sanaa kuona MAMA yake anafunga ndoa na kuwa mke wa mtu sasa.

'Kiukweli mwanangu anakuwa na furaha kusikia Mama yake nataka kugunga ndoa tena yeye amekuwa akinitania kwa kuniita jina la BI Harusi mtarajiwa”

amesema kuwa atafanya send off na kitchen Partry siku moja ambao yeye ameipa jina siku hiyo kuwa ni NATASHA NIGHT ataitumia siku hiyo kupata mafunzo ya kuishi vizuri na Mumewe pamoja na kuanza maisha mapya akiwa katika ndoa,mbali na yote hayo Natasha anahofia kufundwa na Bichau japo anahitaji sana elimu hiyo ili impatie mwanga mzuri wa kuishi katika ndoa.

Jambo ambalo limekuwa geni kwangu ni kusikia kuwa MAMA wa MoNALISA alimzaa mwanae huyo Monalisa Akiwa na umri wa miaka kumi na miwili.

Na sasa wanaonekana kama mtu na rafiki wakiwa pamoja au kama mtu na mdogo wake kwa namna wanavyoonekana na kupendezana .

0 comments:

Post a Comment