Friday, January 11, 2013

JKT Ruvu tulifanya makosa





Na Kitalima Gerald 


KATIBU wa JKT Ruvu David Ngaga  amekili kuwa katika mzunguko wa kwanza wa Ligi timu ya JKT Ruvu ilifanya makosa katika mechi  mbali mbali ilizocheza .

Akizungumza na Champion jumatatu  David Ngaga amesema wamebaini  makosa mbalimbali  katika mechi walizopoteza msimu wa kwanza wa ligi na kuamua kufanya usajili katika dirisha dogo na kuongeza wachezaji watano katika kikosi cha JKT Ruvu .
“Tulifanya makosa mwanzo hatukua na viungo washambuliaji wakutosha lakini tumetambua makosa  na wachezaji wametambua makosa yao hali hii ndio imepelekea kuwaongeza washambuliaji  wengine watano katika kikosi cha JKT Ruvu akiwemo Mussa Mgosi na Zahoro Pazi

“Mbali na kina mgosi kuna Kiungo mshambuliaji wa kushoto Immanuel Pius,Nashoni Naftal na Beki Kisimba Rwambano ambao teyari wamekwisha anza mazoezi chini ya Kocha  Charles Kilinda

Katibu David amesema kuwa anatambua  JKT Ruvu inakibarua kikubwa kutokana na makosa yaliyotendeka lakini anaimani kubwa sana kuwa kwa kikosi walichonacho sasa wanaweza kupata zaidi ya points saba.

“kwa sasa JKT Ruvu tumejipanga kupata points saba zaidi na kwa kikosi chetu cha sasa naamini hakuna litakaloshindikana  maana wachezaji wanajiandaa vyakutosha kwa  msimu wa pili wa Ligi  huku wakijua ni nini wakifanyacho.

JKT Ruvu walifungwa magori 3-0  na Azam FC walipocheza mechi ya kirafiki  Katika uwanja wa Chamazi Kabla Azam FC hawajaelekea Zanzibar kwa mashindano ya Mapinduzi.

0 comments:

Post a Comment