Friday, January 11, 2013

Harakati za Uchaguzi Premium League zaiva




Na Kitalima Gerald 

MWENYEKITI kamati ya Uchaguzi TFF lyatto amesema kuwa mchakato wa kuwatafuta viongozi wa Tanzania Premier League Board umeanza rasmi na uchaguzi utafanyika tarehe Ishirini na mbili mwezi wa pili jijini Dar es salaam.

Akizungumzia nafasi  za kugombewa ni pamoja na Mwenyekiti wa TPL Board,Makamu Mwenyekiti wa TPL Board,pamoja na Wajumbe wawakilishi wa Klabu za Ligi Daraja la Kwanza kwenye Kamati ya Uongozi ya TPL Board ambazo ni nafasi mbili.

“Fomu za maombi zitaanza kutolewa tarehe kumi na nne mwezi huu kutoka kwa Katibu wa Kamati ya uchaguzi ya TFF(Katibu Mkuu)  na mwisho wa kuludisha fomu ni tarehe kumi na nane ya mwezi wa kwanza,fomu ya mwenyekiti  na makamu Mwenyekiti itaghalimu Shillingi Laki Mbili wakati fomu ya Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TPL ni Shillingi Laki MOja.






0 comments:

Post a Comment