Na
Kitalima Gerald
MWENYEKITI kamati ya Uchaguzi TFF Deogratias lyato
amedai kua Katiba ya TFF haimzuii Kiongozi yeyote yule aliyepo Madarakani
kugombea nafasi yoyote ile katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF.
Lyato
amesema kuwa hakuna kipengele chochote
kile katika katiba ya TFF kinachotoa pingamizi kwa kiongozi aliyopo madarakani
zaidi ya mara mbili kugombea tena nafasi yoyote ile katika shirikisho hilo.
“hakuna
kipengele chochote kile katika katiba ya TFF kinachoweka pingamizi kwa kiongozi
yeyote aliyopo madarakani kwa mara kadhaa kugombea nafasi kwa mara nyingine
tena ila kunakipengele kinachozuia mtu akiwa na umri chini ya miaka ishirini na
nne (24)
“kwa
upande wa mgombea wa Uraisi TFF ikiwa mgombea amezidi Umri wa miaka sabini na
tano (75) katiba hamruhusu kugombea, mbali na kigezo cha Umri hakuna kipengele
kingine kinacho mzuia mtu kugombea nafasi yeyote ile katika shirikisho la mpira
wa miguu Tanzania”
Lyato
imebainisha kuwa kama kuna kiongozi yeyote yule aliopo madarakani kwa sasa au
kaongoza shirikisho hilo kwa mara kadhaa ikiwa hata gombea katika nafsi za
uongozi katika uchaguzi utakaofanyika 24 mwezi wa pili mwaka huu utakua ni
utashi wake mwenyewe kutogombea kama kigezo cha umri hakijawa pingamizi kwake.
“kiongozi
yeyote yule aliyopo madarakani kwa sasa katika Shirikisho la Mpira wa miguu
Tanzania kama hatogombea basi ni utashi wake mwenyewe kutogombea “







0 comments:
Post a Comment