Thursday, January 12, 2012

GOLDEN RING-PETE YA DHAABU.


Mwandishi: GERALD KITALIMA

TELEPHONE NUMBER:0717-199561




            Badra na basil ni wanafunzi wa chuo kikuu cha st.agustine mwanza,wakiwa chuoni hapo basil hufahamika sana kwa walimu na wanafunzi wenzake sababu ya fani yake ya kuimba yaani ni msanii mwimbaji,hali hii ilimpelekea kupendwa na vijana wengi wa jinsia zote hapo chuoni na baadhi ya walimu walio tambua kazi na mchango wa basil katika kuwakusanya raia na kuwapunguzia stress za maisha pale awapo stejini akiimba nyimbo zake hata kufanya copy ya nyimbo nyingine za wasanii wengine.

Badra hakuwahi hisi wala kuzania kama siku moja anaweza kuwa kalibu na basil hata kwa kupiga stori tuu,hii inaonesha jinsi gani basil alikua mtu wa dhamani kwake yaani kifupi badra alijihisi kuwa yeye asingekua na hadhi hata ya kuongea na basil.laahasha usilolitambua ni sawa na usiku wa giza,badra alikua na utamaduni wa kwenda club na katika kumbi mbalimbali za starehe ifikapo week end,hivyo basi siku ya jumamosi kulikua na tamasha basil aliudhulia tamasha hilo kama mwanafunzi na wala si msanii akiwa na jamaa zake wakipeana support kushangweka kiujanja zaidi.

Badra pia alihusika kwa namna moja katika tamasha hilo hivyo alitokelezea kwa lengo la kula bata na kupunguza stress za masomo badra hakuwa alone nae alifuatana na mashostito wa town wanaotokea pande za college mpaka hapo najua ushawajua kuwa ni masister duu ndio nawazungumzia,lakini cha ajabu makundi yote mawili yalifika muda sawa na wakiwa wamechelewa tulipo waona kwa mbali tulijua wametokea kiwanja kingine hapa wamefika kumaliza shughuli tuu,lakini kadili walipo sogea ndipo tukabaini kuwa hakukua na uhusiano wowote ule kati ya kundi la masharobaro wa college na masister duu wetu wa chuo.

Kwa ule muda waliofika viti na meza zote zilikua zimesheeni raia wa kutosha,wakiwa katika hali ya kutahamaki mhudumu alikuja na meza moja na kuwawekea pale na kuwaambia kuwa itawabidi wa share meza kwani ndiyo ilikua meza ya mwisho,haikua ngumu kwao sababu kusudio lao ni kula bata ndefu,waliletewa viti na kuhudumia vinywaji,baada ya vyombo kuanza panda kichwani ndipo ulikua wakati wa kutambulishana na kufahamiana vizuli,badra alijikuta akipiga stori na mtu ambae kamwe hakuwaza kama ingekuja tokea hata wakaongea kwani yeye alimuona kama mungu mtu kwa jinsi basil alivyokuwa akiji brand mwenyewe.

Hii ilikua ni nafsi ya kila mmoja kufahamiana na wenzake na kubadilishana mawazo,hapo ndipo urafiki ulipo anza kati ya basil na badra wakiwa chuoni na hii ndiyo ilikua tiketi ya mahusiano kati ya wawili hawa,baada ya maongezi ya muda mrefu walibadilishana number za simu,lakini nafsi na roho ya badra ilitawaliwa na furaha ndani yake kama ameokota fuko la mshahara,jamani nadhani tunajua pindi tupatapo nafasi ya kuwa kalibu na mtu ulie hisi huwezi pata nafasi ya kuwa nae kalibu kutokana na umalufu wake bhanaaa.

Mawasiliano ya kalibu yalijengeka kati ya wawili hao ndani ya siku tano tuu,weekend iliofuata basil alimualika badra chakula cha jioni,siku ilipowadia basil alimkumbusha badra na kukubalina saa kumi na mbili na nusu wakutane sehemu husika,basil aliendelea na majukumu yake ya kila siku kwani alikwenda studio kwanza kuingiza vocal tetemesha records chini ya producer wake kidbway,lakini ratba ya kuingiza vocal ilihalibika kwani akiwa studio walitokea wanamuziki kutokea dsm wanaume family hivyo walitaka kufanya truck na kuondoka siku inayofuata na kuicha ikiendelea andaliwa.

Basil aliambiwa na kidbway asubili kidogo asiondoke,alisubili kwa muda mrefu bila mafanikio hivyo alilazimika kumtoloka producer wake ili akatimize malengo yake ya kuonana na badra,lakini hat hivyo kwa muda aliotoka alihisi angechelewa,hakuwa na budi kukodo boda boda ili aepuke foleni njiani,akiwa njiani basil alipata ajali ya pikipiki aliumia na kupelekwa hospitali ,akiwa njiani na katika maumivu makali aliota simu yake na kuwaomba watu wampe taalifa badra kuwa amepata ajali na anaelekea hospitali.

Badra alishtushwa na taalifa ile hivyo alichanganyikiwa na kuuliza mambo mara nne nne,ahhha kwa hiyo hajaumia sanaa,vipi yupo hospitali gani,jamani saa ngapi kapata ajali mbona mimi nimeongea nae kwenye simu,pindi yanaulizwa maswali haya badra alikua akionesha alikua anabubujikwa na machozi kwani promise imegeuka maumivu moyoni mwake kwa kupata taalifa isiyo nzuli kwa yule ampendae kwa dhati.badra alichukua jukumu kuhakikisha anafika hospitali usiku ule,akiwa katika hali ya sintofahamu alifanikiwa kufika hospitali kumuona basil akiwa poa kiasi baada ya kupewa matibabu……………itaendelea

0 comments:

Post a Comment