Thursday, November 24, 2011

serikali ya wanafunzi ni toroli bovu



                                                                                                                                                                        Serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha tumaini university dar es salaam TUSODARCO,Naifananisha na toroli bovu lisilo tembea na lililo shindwa kubeba mzigo na kuelemewa na mzigo mzito.

Hii inajidhirisha wazi kutokana na uteuzi mbovu wa viongozi katika serikali hiyo,kuanzia ngazi ya chini  ya uongozi mpaka ngazi  ya juu uongozi   katika wizara zake,kwani uteuzi huo ndio umekua chanzo cha mambo mengi kushindwa  kufanyika, hata kama hufanyika  lakini haku  kidhi haja na mahitaji ya wanafunzi,hii si mara ya kwanza kwa kiongozi mkuu wa serikali hiyo kufanya uteuzi mpya katika baadhi ya wizara kwani awamu ya kwanza alimtoa madarakani waziri wa mikopo na kumpa wadhifa  huo mtu mwingine,kama kweli mh:Rais uliamua kuchukua jukumu zito kama hilo hukutambua toka awali kwamba waziri huyo hakuwa na vigezo vya kuwa waziri wa bodi ya mikopo?

Chanzo changu cha habari kinanipasha kuwa,Rais wa serikali ya wanafunzi amekua na silka,hulka ya kuteua viongozi kwa kuzingatia”USWAHIBA”,kwa hali hii mkuu wangu hutaweza kusukuma kurudumu la maendeleo kwa wanafunzi wa tumaini university kama inavyofahamika huwezi kuwa mtendaji mzuri wa shughuli za kiserikali ikiwa boss wako ni jamaa yako,utafanya uzembe,makosa lakini mwisho wa siku hawezi kukudhuru kwa jambo lolote lile,nakukumbusha tu wazungu husema,
THE BEST FRIENDS ALWAYS IS THE ONE WHO LET YOU DOWN,hili kichwani likuingie mh:Rais.

Nikukumbushe tuu mh: wanafunzi walikua na imani kubwa sana na uongozi wako kabla hujaingia madarakani wakijua kuwa utakua mtetezi wao kwa matatizo yao,lakini mambo yamebadilika kwao kwa sasa,wanafunzi walianza kuwa na mashaka na serikali yao pindi tuu ulipotangaza baraza lako la mawaziri na serikali yako kiujumla ,imani ya wanachama wako umeichoma na kuiteketeza kwa maamuzi yako mwenyewe na washauri wako kwa kuwaacha watu dhabiti na wachapa kazi mahili na kuamua kukumbatia gunia lenye misumali linalo kupa maumivu makali.

Nini maana ya serikali yako ikiwa siri bayana zinawekwa wazi,na mambo yasiyo ya siri etii yanafichwa,mfano ulishawai kutaka kuwasimamisha kazi baadhi ya viongozi wako kwa kuwapa barua,sisi kama wanafunzi hatukupashwa kujua kama umetoa vitisho kwa watu hao sababu hawakufuata matakwa yako,hii inaonesha ni jinsi gani team yako haina watu dhabiti kusimamia shughuli za serikali na uongozi kiujumlaa,mh leo unakosa imani na viongozi uliowateua mwenyewe na kuwaapisha mbele ya kadamnasi kwamba watalinda na kutetea masrahi ya wanafunzi na serikali yako?huoni unatupa picha kuwa haukuwa makini wala hukujali masuala ya msingi katika kutengeneza team work yako?mh:Rais uongozi si kupuliza filimbi,japo hata kupuliza hiyo filimbi zinahitajika sifa na ujuzi ili uweze kupuliza vizuri.
nashindwa kuelewa inakuaje  viongozi wako leo wanakusaliti?au kunajambo haliendi sawa?haya ni maswali yangu kwako na serikali yako kiujumla ,unawezaje kumtoa  mbwa ndani na kumkalibisha  chui?hao washauri wako kweli wanania nzuli na serikali yako?

Tunakumbuka ahadi zako mh: sijajua mpaka sasa umetekeleza kwa asilimia ngapi sababu hakuna mawasiliano kati yetu sisi wanafuzi na serikali yako na kama yangekuwepo basi tungepewa hata feed back juu ya utekelezaji  wa ahadi zako  kipindi cha kampeni ,si kama sina jicho kuona mazuli machache yaliyofanywa na serikali yako laaahasha:ila nimekua na jicho kama lako kututeulia viongozi wasiojua dhamana yao kama viongozi wa serikali ya wanafunzi.

Siku zote mambo mazuli huigwaaa napata wakati mgumu sana kuona uongozi ujao utaiga nini na kujifunza nini kutoka katika serikali yako,serikali yako naifananisha na serikali kuu ya tanzania kwani mambo ya akina jairo,luhanjo hayakosekani katika serikali isiyona udhubutu,si kana kwamba wanafuzi ni wajinga hapana ila wanaitaji busara zako katika kuiendesha serikali yako,

Katika serikali yoyote ile fursa zinapopatikana huwa ni kwa maslahi ya wanafuzi wote na si kwa kundi flani la watu kwa maslahi ya  watu wachache,inakuajee fursa hizo kuwapata viongozi wako tuu au watu wakaribu na viongozi wako?ikiwa unatambua vizuri slogani yako UNITY FOR CHANGE mh Raisi tunaitaji mabadiliko.


0 comments:

Post a Comment