Monday, October 28, 2013

SIMBA ,AZAM MAKOCHA WASHINDWA KUTAMBIANA

Masaa kadha yakiwa yamesalia kwa vinara wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Simba kukutana na Azam FC katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaam, makocha wa timu hizo wameshindwa kutambiana.
 
Imezoeleka kwa kila Timu zinazoingia Dimbani kupeana vigambo vya hapa na pale kwa kuoneshana ubavu kabla hata ya kuanza kuchezwa kwa mechi hizo lakini hali imekuwa tofauti kwa mechi ya Simba na Azam Fc ambao leo wataingia Dimbani kuchuana

Simba inatarajiwa kushuka uwanjani kwa tahadhari kubwa, kwani endapo itakubali kipigo itapoteza uongozi wa ligi hiyo kutokana na kuwa na pointi sawa na Azam lakini vinara hao wakiizidi kwa wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Kama ilivyo kwa Simba, Azam nayo itahitaji kuibuka na ushindi ili kukaa kileleni mwa ligi hiyo yenye upinzani mkali tofauti na msimu uliopita.

Katika msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14, Simba, Azam na Mbeya City, zote zina pointi 20, lakini Wekundu wa Msimbazi wapo kileleni kutokana na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa, wakifuatiwa na 'Wanalambalamba', huku wakali hao wa Mbeya wakishika nafasi ya tatu.


0 comments:

Post a Comment