Monday, September 2, 2013

PICHA 15 SHOW KALI YA KILL MUSIC TOUR KIGOMA ILIVYOFANA KWELI HAKUNA KIGOMA BILA DIAMOND


Umati wa mashabiki waliojitokeza kwenye tamasha la Kili Music Tour, wakifuatilia onyesho hilo lililofanyika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.
 MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Diamond Platnum juzi alifanya kazi kubwa katika tamasha la Kili Music Tour lililofanyika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika Mjini Kigoma.


tamasha hilo lililohudhuriwa na umati wa mashabiki, waliokuwa wamejawa na furaha kuwashuhudia wakali wa waliofanya Vizuri katika Muziki kwa Mwaka 2012.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Naseeb Abdul ‘Diamond’ akifanya yake katika tamasha la Kili Music Tour lililofanyika Kigoma.
Diamond alifanya onyesho la aina yake na kuwafanya mashabiki kumshangilia kwa kelele mno kiasi kwamba kutounesha utaofauti wa kauli kuwa nabii hakubaliki nyumbani kwani kwake ilikuwa ni Tofauti mno.
Diamond ambaye alikuwa msanii wa mwisho kupanda kwenye jukwaa, aliwaita wasanii wenzake ambao ndio wenyeji wa Kigoma kama Recho, Mwasiti pamoja na Linex na kuimba wimbo wa Leka Dutigite na kuwaamsha mashabiki waliofurika Uwanjani hapo.

Wasanii wengine ambao walitumbuiza katika onyesho hilo lenye ujumbe wa ‘Kikwetu Kwetu’ ilikuwa ni pamoja na Lady Jaydee, Barnaba, Ben Pol, Izzo Bizness, Recho, Prof. J, Fid. Q, Roma, Mwasiti, Linex pamoja na Kala Jeremiah.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Izzo Bizness akiwapagawisha washabiki katika tamasha la Kili Music Tour lililofanyika juzi kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma


Diamond akiongoza wasanii wenzake Mwasiti, Linex na Recho katika nyimbo ya ‘Leka Dutigite’ na kuwaamsha mashabiki waliofurika uwanja wa Lake Tanganyika katika tamasha la Kili Music Tour, mjini Kigoma.





0 comments:

Post a Comment