Monday, September 2, 2013

MAJINA YA WAUZA DAWA ZA KULEVYA WAPO WABUNGE WA CCM NA CHADEMA

Mbunge wa Nzega (CCM), Dk. Khamis Kigwangallah, amesema amepokea majina ya wabunge, viongozi wa serikali na wafanyabiashara maarufu ambao ni wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Dk. Kigwangallah ambaye anataka kuwataja bungeni na watu wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, amesema baada ya kukabidhiwa majina hayo kutoka kwa wananchi, anafanya uchunguzi na kupata ushahidi ili kujiridhisha kabla hajachukua hatua ya kuwataja.

Miongoni mwa majina ya wabunge aliyopewa wamo kutoka CCM na Chadema, na wafanyabiashara maarufu wote wanatoka mkoa wa Dar es Salaam.




0 comments:

Post a Comment