Thursday, August 15, 2013

MKURUGENZI WA BENK YA CRDB ABULUZWA MAHAKAMANI.


Mkurungenzi wa Benki ya CRDB katika tawi la Moshi amebuluzwa mahakamani na kufunguliwa shitaka la kufanya kosa la Uzalilishaji wa kijinsia dhidi ya mteja wa benki hiyo ambae amefahamika kwa jina la Lulu Kajembe...!

Mkurugenzi huyo Bw Francis Mollel alipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kilimanjaro kwa kosa la kumtukana na kumtolea maneno ya Kashfa Lulu Kajembe wakati amepanga foleni .

Shauri hilo la jinai namba 365 lilifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo jana chini ya Hakimu Swai.

Mshtakiwa alikana shtaka hilo na kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 21, mwaka huu itakapoanza kusikilizwa.

0 comments:

Post a Comment