Thursday, December 5, 2013

NAHITAJIKA KLABU KUBWA NJE YA AFRIKA-SAMATTA

Mshambuliaji matata Mbwana Samatta ambaye Juzi aliiwezesha Kilimanjaro Stars Kushinda gori moja dhidi ya Burundi katika Mechi ya Mwisho ya Makundi
amefunguka na kuweka wazi kuwa Kuna Timu nyingi za Ulaya Zinamuhitaji kwenda kuzichezea.

Mshambuliaji huyoambaye kwa sasa katika Kikosi cha Kilimanjaro Stars amesema kuwa hatakuwa na muda Mrefu atatimuka na kwenda kutoa huduma wanayoihitaji ya soka katika Vilabu hivyo ingawa hakutaka kuweka wazi Klabu ambazo zinahitaji huduma yake huko Ulaya kwa sababu ya Kuheshimu Mkataba wake na TP Mazembe.

"Ningekutajia klabu na nchi inayonihitaji, mimi bado nina mkataba na TP Mazembe na huwa haituruhusu kuongea na vyombo vya habari masuala ya mikataba yetu. Nikifanya hivyo nitachukuliwa hatua ila kweli ninatakiwa na klabu kubwa nje ya Afrika,"

0 comments:

Post a Comment