Tuesday, May 14, 2013

MB DOGGY AMERUDIA MAKALI YAKE


Msanii Mb Doggy alietamba katika miaka ya 2001 na ngoma kibao kali zikiwemo Latifa,Siunajua na ngoma zingine kibao na kupotea katika tasnia ya bongo fleva baada ya kuingia kufanya biashara zake mwenyewe za vinyago amerudi tena kwenye game ya bongo fleva na makali ya miaka ile.

Katika siku za hivi karibuni i Mb Doggy aliamua kuludu katika kazi yake ya muziki iliyompa jina mjini na mafanikio kadhaa na kuamua kufungua studio ya kwakwe mwenyewe ilikwenda kwa jina la Makopa japo hatukusikia kazi yoyote kutoka katika studio yake hiyo lakini sasa ameachia kibao kipya kinachokwenda kwa jina la MA-DIGINA .

Katika Joint hii mpya ya MB Doggy ameonesha ukari wake wa kuimba na kucheza na sauti nzuri na maneno yenye ladha ya kusikilizika kama ambavyo alikuwa akifahamika katika ngoma zake zote alizofanya poa miaka ya nyuma.

mapenzi ya vita unahasira jawabu hasara wengi wao unawakuta wanaumia hawana subira”ni moja ya mistari iliyomo katika wimbo huo

0 comments:

Post a Comment