Madam
Rita Paulsen ambae ni Chief Judge katika shindano la BSS amesema kifo
cha Mwanamuziki Albert Mangwear ambae amefariki jana kutokana na
matumizi ya madawa ya kulevya nchini South Africa ni Pigo katika
Tasnia ya Muziki nchini.
“Kifo
cha Albert Mangwair kimenisikitisha sana. Alikuwa ni rafiki yangu na
pia tumeshashirikiana kwenye kazi mbalimbali. Kifo cha Ngwair ni pigo
kubwa kwa tasnia ya mziki. Natoa pole kwa familia, rafiki, mashabiki
na wadau wote wa hip hop”
Albert
Mangwear ni kati ya wasanii wachache wa Hip Hop Nchini walioweza
kufanya muziki wa Hip Hop kwa Style ya Pekee na kuweza kuwakilisha
vizuri Hip Hop kwa Tanzania,alishafanya ngoma kibao ambazo
zitaendelea kuishi katika maisha ya kawaida kutokana na aina ya
ujumbe uliopo katika nyimbo hizo.







0 comments:
Post a Comment