Tuesday, March 6, 2012

MADAKTARI WANA MOYO WA KAZI

mwanaharakati Bw Renatus mkinga akifunguka
madaktari wana moyo wa utendaji kazi na kuokoa maisha ya watanzania wanaosumbuliwa na magonjwa mbalimbali,hili limethibitishwa na mwanaharakati na mtetezi wa wanyonge BW Renatus MKINGA ,
akiwa anazungumza na kituo kimoja cha television jijini dare salaam leo asubuhi mwanaharakati huyo amesema madaktari wanamoyo wa utendaji kazi bali serikali pamoja na viongozi wamekua chanzo cha matatizo mbalimbali katika hospitali za hapa nchini,hivyo kuwakatisha tama na moyo katika utendaji wao wa kazi.

‘’Jamani mimi nililazwa pale MUHIMBILI hivyo nimeshuhudia jinsi madaktari walivyo makini na kazi yao kwa kuwasaidia wagonjwa ili waludi katika halizao za awali,sema sasa MUHIMBILI vifaa hakuna,madawa hakuna,mashine za kufua mashuka ni mbovu,film x ray hakuna jamani katika mazingira hayo sasa madaktari wanafanya nini? Hili nalo ndilo moja ya vitu vinavyowafanya wagome madkati wetu sababu anakosa ufanisi wa kazi kutokana na kukosa vitendea kazi,serikali ipo wap?”

Akiongezea ,mkinga alidai kuwa madaktari wanaingia katika mgomo tena hiyo kesho sababu kubwa serikali imeshindwa kutekeleza makubaliano yao yakutaka viongozi wajuu katika sekta ya afya akiwemo waziri wa afya na naibu wake, kuwawajibishwa kutokana na kuleta mkologano wa mambo.


ni masaa kadhaa yamebakia  madaktari kuingia katika mgomo,yaani ni muda mfupi umebakia watanzania tunaanza kupoteza ndugu zetu kwa kukosa huduma pindi wafikishwapo hospitali hii yote ni sababu tu wa watu wachache tuu wenye nia ya mbaya na uroho wa madaraka, 

MUNGU IBARIKI TANZANIA,

0 comments:

Post a Comment