Wasanii
wa bongo fleva wanaofanya poa kunako muziki wa kizazi kipya Diamond
Platnumz, Vanessa Mdee na mfalme wa hip hop, Joh Makini watafanya
Show kali
kwa vijana katika majiji ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya,
Arusha na mji wa Moshi kuanzia Jumapili hii.
Maurice
Njowoka alisema kuwa kazi hiyo ya kutoa burudani kali kwa vijana
itaanza rasmi kwenye fukwe za Coco jijini Dar es Salaam Jumapili huku
Diamond na wakali wenzake wakikonga nyoyo za wapenzi wa muziki wa
kizazi kipya ambao watapata burudani bure bila ya kulipa viingilio.
"Lengo
la burudani hii ni kutoa fursa kwa vijana, hasa ambao wamekuwa
wakikosa burudani za aina hii kwa kushindwa kulipia viingilio,
kufurahi pamoja na marafiki zao huku wakiburudika na bidhaa zetu,"
alisema Njowoka huku akiwaomba vijana kujitokeza kwa wingi Dar es
Salaam Jumapili na maeneo mengine ambako kampeni hiyo itawezeshwa na
kampuni yao.






0 comments:
Post a Comment