Baada
ya kuondolewa katika Nafasi ya juu kabisaa Simba Sports Club ambayo
kwa sasa inakamatiwa na Azam Fc ikifuatiwa na Mbeya City huku Simba
ikichukua nafasi ya NNE Kocha wa Simba Kibadeni amefunguka na kusema
kuwa watamaliza Mzunguko wa kwanza wa Ligi kwa heshima.
Kikosi
cha Simba jana jioni kilitarajiwa kuingia kambini Bamba Beach,
Kigamboni kwa ajili ya kujiandaa na mechi yake ya kesho dhidi ya
Ashanti United.
Kibadeni alisema wachezaji wake wanaendelea vizuri na mazoezi huku kila mmoja akijipanga kucheza kwa juhudi kwa lengo la kupata pointi tatu muhimu.
"Tuko vizuri na tunaamini tutamaliza kwa heshima, msimu huu tulipanga kujenga timu, lakini hapa tulipofika si pabaya, tumefungwa mechi moja tu," Kibadeni alisema.







0 comments:
Post a Comment