Msanii
aliyevunja rekodi kwa kupata Tuzo nyingi kwa mara moja kwa mwaka
2011-2012 Mpaka sasa Mfalme wa Kimanzichana, Hamis Abbas
Kinzasa
‘20%’ ameamua kurudi na kumaliza tofauti yao kati yake na
Produza aliyetengeneza Ngoma nyingi zilizomuweka kileleni Mkali huyo
ambaye anafahamika kwa jina la Man Water.
Toka
walipotofautiana na Mtayarishaji huyo Msanii 20% hajawahi kufanya
kazi ambayo ilifanikiwa kumrudisha tena katika Ramani ya muziki na
kuwashika Mashabiki kama ilivyokuwa awali.
Lakini
tunaamini kuwa Msanii huyo amejifunza jambo hivyo hatutegemei kusikia
suala kama hilo limejirudia tena kwa wawili hao kuingia katika
tofauti kwa kosa ambalo lilijitokeza mwanzo.
Niwatakieni
mafanikio mema na imani yangu ni kubwa kuwa Man Water atafanya kazi
ya kumrudisha Msanii 20% kwani hata mtoto akichafua kiganja chako
unachofanya ni kusafisha na maisha yanaendelea na si kukata kiganja.







0 comments:
Post a Comment