Friday, October 25, 2013

MRISHO NGASA,HAMISI KIIZA WAUNDA BENDI 'DANGER ZONE'

Winga wa Yanga na timu ya Taifa Mrisho Ngasa amefunguka na kusema kuwa ushirikiano mzuri wanaouonyesha wakiwa uwanjani kicheza sambamba na Hamisi
Kiiza, umepeleke wao kuunda Bendi yao inayokwenda kwa jina la 'Danger Zone'.
 
Kwa sasa tuna 'kombinesheni' (muunganiko) kali kwenye safu yetu ya ushambuliaji ambayo tumeamua kuiita Bendi ya 'Danger Zone' kwa sababu mimi na Kiiza tunapokuwa kwenye eneo la hatari muda wowote tunafanya maajabu," alifafanua Ngasa.

Ngasa ambaye ameifungia Yanga mabao matatu katika mechi tano alizocheza msimu huu tangu atoke kifungoni huku akitoa pasi tano za mwisho, anaamini kujituma kwake mazoezini na kwenye mechi ndiko kunakomfanya ang'are katika kikosi cha klabu yake msimu huu wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

"Namshukuru Mungu kwa kunisaidia kufanya vizuri licha ya kuandamwa na jambo zito la kusimamishwa kucheza mwanzoni mwa ligi na kulipa mamilioni ya shilingi.

(Nukuu zote chanzo:Nipashe)



0 comments:

Post a Comment