Wednesday, September 4, 2013

SIKULAUMU DAYNA NAMPONGEZA SHEDDY CLEVER NA DIAMOND KWA KUTIMIZA MALENGO.

Malengo ni jambo moja kubwa na jambo la msingi sanaa ambalo binadamu wote tunapaswa kujiwekea na kusimamia ili yatimiye.Nakumbuka siku ya kwanza...!
nafanya Interview na Produza Sheddy Clever akiwa katika studio yake pande za Tabata aliniambia Moja ya ndoto zake nikuona anafanya Wimbo Mzuri na Diamond Platnum siku moja.

Baada ya muda kupita nilisikia kuwa ameanza kufanya kazi na Msanii ambae alikuwa akiwaza siku moja kufanya nae kazi, hatimae lengo lake limeweza kutimia kwani amefanikiwa kufanya kazi nzuri ambayo inazungumziwa na watu wengi na kuhusishwa na kuibiwa kwa Beat.

Nijuacho mimi katika Wimbo wa My Number One Msanii pamoja na Produza wameshirikiana vizuri kutengeneza kitu kizuri,Suala la Beat ilikuwa ya Dayna au sijui ilikuwa ya Nani sio hoja ya kusimamia kwani miliki ya Muziki ni ya Produza,kazi ya Msanii ni kuimba,kutunga mashairi,na kutafuta style nzuri ambayo itabamba watu na kazi ya Produza ni kutengeneza Muziki.
Inanishangaza Msanii anaibuka na kusema kuwa Muziki au Beat ni mali yake ,Najiuliza ni yake kwa misingi ipi?
Nijuacho mimi Muziki ni mali ya Produza ila kama msanii amebuni Melody,Tone na style ya uimbaji hivyo ni mali yake yeye pamoja na Mistari iliyopo katika Wimbo husika.
lakini suala la Beats au muziki huo ni ubunifu wa Mtu mwingine ambae ni produza,Sasa iweje Dyana useme Sheddy Clever ameuza beat yako kwa Diamond?Je! Sikiuzi wewe ni Produza wa Muziki kwamba ulikaa ukaumiza kichwa chako na nguvu yako kutengeneza huo muziki? 
 
Mimi naamini kuwa Muziki ni mali ya Produza kwakuwa ametumia ubunifu wake na akili yake kutengeneza huo mdundo ambao wewe unasema wa kwako.

Na wewe ulifanya kazi yako ya kubuni Melody na Tone ya Wimbo wako ili mwisho wa siku ngoma iweze kusikika vizuri hivyo leo ungeibuka na kuniambia Diamond ameiba wimbo wangu kitu cha haraka kusikiliza kwangu mimi ni Melody,Tone na Style ya Uimbaji zilizotumika katika Nyimbo hizo pamoja na uandishi maana ndicho unachomiliki Msanii lakini huwezi sema Diamond Platnum kaiba wimbo wako kisa Beat zinafanana sasa hapo amekuibia nini?



Katika Nchi za wenzetu ni Wasanii wachache sanaa ambae anaweza kuingia studio na kulipa Pesa yake mwenyewe ili akatengenezewa Wimbo na Produza Ndio maana wengi wao wanaishia kuwa Chini ya Lebo fulani na muziki wa Huyo Msanii unakuwa chini ya Lebo husika na si mali ya Msaniii.
Kuna kila haja Wasanii wetu wa Bongo kuitafuta Elimu ya muziki tuufanyao ili kujiongezea uelewa na maarifa zaidi.









0 comments:

Post a Comment