Thursday, May 23, 2013

SIJAWAHI KUUZA MATUNDA -BEN PAUL




Msanii wa muziki wa Rnb pande za Bongo anaetamba na Hits Song kibao japo kwa sasa kwa ngoma yake ya Jikubali amezidi kujiongezea mashabiki rukuki kutoka kila pande ya Nchi amekataa kuwa alishawahi jishughulisha na biashara ya kuuza matunda.

Ben Paul alikuwa ndani ya Tinga namba moja kwa vijana kupitia ukurasa wa Facebook akibadilishana mawazo kwa kuchat na Fans zake kupitia KIKAANGONI LIVE CHAT.alipohojiwa na moja wa Fans wake kuwa alishawahi kuuza matunda alisema kuwa hajawahi kufanya biashara hiyo kwani muda mwingi aliutumia kimasomo.

'”Hahaha si kweli, maisha yangu kabla ya muziki yalikuwa shuleni tu, 

kuanzia 1997 mpaka 2010”

kwa mujibu wa Ben Paul amesema kuwa mbali na muziki kwa sasa anasoma na kufanya biashara zake za hapa na pale zinazomuwezesha kuendesha maisha yake na familia yake kiujumla na kumfanya kuendelea kuwa Ben Paul,

baada ya kutaka kujua mpango wake katika muziki Ben PAUL alieleza kuwa anampango wa kuanzisha Band ya kwake mwenyewe ambayo atakuwa akiitumia kufanya nayo kazi na kufanya Live Shows kwa Band yake mwenyewe ambayo anatarajia itakuwa teyari mpaka itapofika mwezi September.

ndio nina mpango wa kufanya collabo na wasanii wakubwa kimataifa na nimeshaanza kuwatumia demos wasanii mbalimbali wa afrika mashariki, natumai nitajibiwa muda si mrefu, kuhusu bendi yes niko kwenye maandalizi mpaka kufikia september mwaka huu naamini nitakuwa nimefanikisha”

0 comments:

Post a Comment