Mwenyekiti
wa Baraza la Mitihani la Taifa-NECTA ambaye pia ni Makamu Mkuuwa Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam,Prof.Rwekaza Mukandala amesema hayuko tayari kubadili
matokeo ya Kidato cha Nne.
Prof
Mkandala ameweka wazi msimamo wake huo kama mwenyekiti wa Baraza la Mitihani la
Taifa na kusema kuwa haoni haja na tija kufuta matokeo ya kidato cha NNE ya
mwaka 2012 kwa kuwa waliptisha Matokeo hayo mbele yao na kwa idhini yao hivyo
haoni sababu ya kufuta matokeo hayo na hata kama yanafutwa ni kwa faida ya nani
na kwa ustawi ya Elimu ya wapi? Alihoji Prof. Mkandala
'Sisi tulipitisha matokeo hayo mbele yao na kwa idhini yao.Iweje leo Baraza libadili matokeo?.Tunafanya hivi kwa faida ya nani na kwa ustawi wa elimu ya wapi?'
'Sisi tulipitisha matokeo hayo mbele yao na kwa idhini yao.Iweje leo Baraza libadili matokeo?.Tunafanya hivi kwa faida ya nani na kwa ustawi wa elimu ya wapi?'
Kutokana
na sakata linaloendelea nchini sasa juu ya matokeo ya kidato cha nne na msimamo
wa serikali kuhusiana na kufuta matokeo ya kidato cha Nne na kutaka
kusahihishwa upya,Mwenyekiti na Katibu Mtendaji Dr.Joyce Ndalichako wanajiandaa
kuachioa ngazi ikitokea Serikali ikisimamia msimamo wake ho wa kufuta matokeo
ya Kidato cha Nne YA mwaka2012.
0 comments:
Post a Comment